Skip to main content

HII HAPA SABABU YA KWANINI MSHAHARA HAUKUTOSHI

 Hebu fikiri kama ungepata kiasi kikubwa cha kujitegemea kufanya mambo yako... je ungeendelea kufanya kazi ya mtu? hapa naamini hata wewe unngeacha kazi... sasa basi ukiona mambo yako kama hivyo yalivyo basi jua uko kwenye mtego wa ajira kwani kamwe mtego huo upo kukufanya uitegemee ajira milele... haya basi na tujifunze sote kupitia makala hii mpya ya uchumi ambayo imeandikwa na:

SOMO LA KWANZA KUHUSU UCHUMI.


Jina: Gwemela Conrad Michael.

Elimu itolewayo: Ujasiriamali na uchumi.

Vitabu vya kuhakiki.

1. Rich dad poor dad by Robert kiyosaki.

2. The power of subconscious mind.

3. The Contagious

4. Art of war by Sitzu.


Mobile number: +255674167126

email gwemelaconrad@gmail.com


Youtube Channel: Brightermango

twitter/instagram: brightermango


Awali ya yote nimshukuru mwenyezi Mungu anayetupa uhai huu wa kila siku na kuturuhusu tuyajue yote tunayoyajua kwa sasa.


Pili; Nimshukuru Mama na Baba pamoja na familia yangu kwa ujumla kutokana na upendo wao wa dhati kwangu kwa kipindi chote cha maisha haya ya upendo wa kweli.


Tatu niswashukuru Marafiki na wapendwa wasomaji wa makala zangu hizi za elimu ya uchumi wa kujitegemea...


Hivyo ni matumaini yangu kuwa Kupitia ushirikiano na ushirikishwaji wa kila pande tutapiga hatua..


  *STORI_YA_ROBERT_KIYOSAKI*

Robert kiyosaki Muandishi wa kitabu cha "Rich_dad_poor_dad" akiwa na umri wa miaka 9 aliwahi muuliza baba yake ambaye alikuwa na elimu ya juu Yaani Ph.D kuwa kwanini shuleni hawatoi elimu ya fedha...na baba yake alimjibu kuwa serikali haijaruhusu wakufunzi watoe elimu fedha...akamuuliiza tena kwanini basi yeye ameamua kufanya kazi ya serikali.... Baba akamjibu kuwa yeye anafanya kazi na alisoma ili afanye kazi serikalini na sio vinginevyo...baba yake akamwambia kuwa lakini asijali kwani yuko na rafiki ambaye pia naye kwake ni baba wa rafiki yake kipenzi aitwaye *Ema*.

Basi Robert akaamua kwenda kwa baba yake Ema na kumtaka awe mwalimu wake kuhusiana masuala ya fedha...

 sababu ya yeye kumuamini mzee yule kwenye masuala ya kifedha ni kwa sababu ya uzoefu wake kwenye nyanja hiyo..... Kwani alianza kujifunza kutoka kwa watu halisi wa kila kitu alichotaka kukifanya.


  ####*WALIMU HALISI NA WASIO*####


Baba yake Ema aliwapoteza wazazi wake akiwa na umri miaka 13 hivyo ilikuwa wazi ni pigo kwenye maisha yake na hivyo alijifunza karibuni kitu kutoka kwa walimu halisi yaani wale wanaofundisha vitu ambavyo wao pia wanafanya... kama vile Wahasibu na uhasibu pia kwa upande mwingine kujua mzunguko wa fedha kutoka kwa mtumiaji wa mwisho na muuzaji wa jumla na pia athari zitokanazo na ukwasi kubaki mahali pasipo na kuondoka.

... Pia alipata na nafasi ya kujua saikolojia iliyopo nyuma ya mafanikio ya kweli na utajiri au ukwasi wa kweli na tofauti kuu kati ya muajiriwa na mjasiriamali mwenye mafanikio ya wazi.



...Je? ROBERT KIYOSAKI alijifunza Nini.

itaendelea!


Comments

Popular posts from this blog

UMUHIMU WA NDOTO.

 Brightermango. KILA MTU ATIMIZE NDOTO ZAKE, SIO LAZIMA WOTE WAWE KAMA WEWE.  Inauma  sana pale unapoona mtu au kundi la watu, wanapoenda kinyume na vile ulivyotamani kuwaona. Kila wakati yamkini ukiwaona unahisi kukwazika, SASA SWALI NI KWAMBA, JE? walipaswa kuwa sawa kama ulivyotaka au walipaswa kufuata matamanio yao binafsi, Ukiepusha ushauri wa mtu kuwa mfuasi wa Iman, au Deen, basi mengine yoote ambayo ni matamanio yetu binafsi hayapaswi kurithiwa na watu wengine, haijalishi ni ndugu, rafiki au hata mtoto wako.  WANASEMA, SIKU HIZI mtoto huyu anafuata mambo yake tu, au Rafiki yangu simuelewi kwani siku hizi hafanani na mimi. WAPO WENGI WANATAMANI KUWAFANYA WENGINE KUFANANA NAO, nafikiri ni kosa la kimkakati linalotokea tangu wazazi wetu wanapotuzaa,kututunza, na kutuongoza sisi ambao ni watoto wao. Iwe kheri kwenu nyote, kwamba, Hakuna Tabia(ndoto) iliyo ya lazima kurithi.  Unaweza kufaulu kumfanya mtu kuwa kama wewe kwa kiasi fulani, lakini kukutana changamoto kama zako akanasa n

MAMBO 4 YA KUACHA SASA ILI UWE MSHINDI.

 Na, Brightermango. MAMBO 4 YA KUACHA SASA ILI UWE MSHINDI.  1. ACHA KUANDAMANA NA WATU WASIO SAHIHI. Maisha haya ni mafupi kiasi kuwa kama tutaruhusu namna yoyote kuwa na watu ambao muda mwingi wanakurudisha nyuma haiwezi kamwe kuwa sawa au na usaidizi badala yake tutaambulia hasara kubwa. Ishara ya wazi  ya watu hao, mara zote wana kuwa na wewe kwenye muda wako wa juu wa mafanikio lakini ukianza kushuka hutomuona yeyote kati yao.   Anza kuandamana na watu sahihi: hawa ni wale tu ambao wanatambua mchango wako na kuelewa zaidi hata kama hujawaeleza kukuhusu. photo: Employment page. 2. ACHA KUKWEPA AU KUKIMBIA MATATIZO YAKO. Saa chache unapokutana na tatizo huwa unapatwa na hofu... lakini kumbuka kadiri unavyojiimarisha zaidi katika kutatua changamoto ndivyo unavyokomaa kukabili nafasi za juu na kubwa hapo mbeleni aidha kwenye ajira au binafsi. ...Jaribu sasa kupambana nayo; Ukweli ni kwamba hata kama ungepaa juu zaidi na kuishi huko ulikokwenda huwezi kukwepa matatizo yanayokuhusu wewe

SIRI|| KUFANIKIWA NI KUSUBIRI.

 Na brightermango. VIPI UMEJARIBU KILA KITU LAKINI  BADO TU UNAKWAMA? Hapana, hujajaribu kila kitu, JE? umejaribu kuendelea kusubiri zaidi. Kuna wakati tunatamani mambo yaliyo juu ya upeo wetu, na tukishauriwa mara nyingi tunagundua hatukupaswa kuyatamani na badala yake kutafuta uwezo kwanza wa kuwa pale kama wahusika, yaani ninachokisema ni kwamba; "TUNAPOTAMANI KUWA KWENYE SHEREHE YA KUHITIMU ELIMU YA CHUO, BASI TULIPASWA KUWA WANACHUO AU WAHUSIKA KWA NAMNA FULANI" au "HUWEZI TUNUKIWA MEDANI KAMA HUKUSHIRIKI MASHINDANO HUSIKA" Basi ndivyo ilivyo kwenye maisha, Yaani ukiyahitaji mambo fulani hapa duniani, jitahidi ujue vigezo vyake ili na wewe uweze kuwa kama vigezo vinavyokutaka. Sasa kwenye hili letu la kujaribu kila kitu lakini bado husogei, Je? Ndio haiwezekani tena wewe kuinuka juu na kufanya mambo yako kwa mafakio? Nifuate kuna kitu leo nitakufunza,... NGOJA TUCHIMBE BUSARA ZA MABABU. Kutoka kwenye kitabu cha THE LIFE, Kinachohusika na uandishi wa