Skip to main content

JINSI WOTE TULIVYO WASIOHAKI...LAKINI TUNAMUHUKUMU MWIZI.

 HIVI UNAFAHAMU KUWA❓


"HATA MWIZI UNAYEMKAMATA BAADA YA KUKUIBIA, NA YEYE PIA ALIKUWA AKIKAMILISHA FURAHA YAKE, SEMA TOFAUTI NA WEWE, YEYE HAWEZI KUVUMILIA MAUMIVU NA KUKUSANYA KIDOGO KIDOGO NA KWAHIVO ANATUMIA NGUVU KUBWA AKILI MBAYA ILI KUPATA PESA AU MALI NYINGI KWA WAKATI MFUPI BILA YA UCHOVU AU MAUMIVU"


matokeo yake yako wazi... Akikamatwa hupatiwa maumivu aliyoyakwepa na hata huchoshwa sana. Kiuhalisia inasemekana kuwa mtu yeyote anayeishi anadhulumu kwa kiasi fulani nafsi au vitu vinanvyomzunguka. Kwa mfano hewa tunayovuta huwa tunaigombania na ndio sababu mapafu yetu hupanda na kushuka IKIWA NI ISHARA YA USHINDANI.


Kwenye utajiri pia, ili mmoja awe maskini, ni lazima yule aliyetajiri amfanye maskini asiwe na elimu...maarifa na zaidi awe na utiifu kwake...kitu ambacho kinafanya sisi kama jamii tuone sawa japokuwa si sawa na ama hakika Mabadiliko ya lazima yanahitajika haraka kwenye jamii yetu.


TATIZO KUU.

"KWENYE JAMII YETU KUNA VITU WAMESHAVIKUBALI NA KUONA VIKO SAHIHI, JAPO KI UHALISIA BAADHI HAVIKO SAHIHI, HII NDIYO WATU HUITA DESTURI... Kwa kawaida watu hukimbilia kusena kuwa "hii ndiyo  desturi yetu.." ili wakamilishe malengo yao" 

 Jamii inalazimisha kuwa,

Maskini haruhusiwi kupata elimu.

Maskini hawezi shiriki maamuzi.

Maskini hapaswi kuonekana sehemu za wazi eti aibu

Maskini eti Ni mtumwa wa tajiri.

Maskini ni wa kukosa haki mahakamani.

Wakati si sahihi na wala si sawa.....


Nafikiri wakati umefika sote tubadilike na kufanya maamuzi sahihi.


Niko natamani wote Tuinuke.... TAJA MAMBO YOYOTE unayohisi jamii imeshayakubali yanayokuathiri kiJAMII NA KIUCHUMI..


TEMBELEA BLOG YANGU GOOGLE KWA KUANDIKA Brightermango...itakuja blog yangu ya kwanza.


imeandikwa na Gwemela Conrad.

CEO.

Brightermango.


photo credit [[ Mary S. Mtui&friend]]


Like my page Brightermango purpose


Nifollow twitter na Insta kama brightermango



Comments

Popular posts from this blog

UMUHIMU WA NDOTO.

 Brightermango. KILA MTU ATIMIZE NDOTO ZAKE, SIO LAZIMA WOTE WAWE KAMA WEWE.  Inauma  sana pale unapoona mtu au kundi la watu, wanapoenda kinyume na vile ulivyotamani kuwaona. Kila wakati yamkini ukiwaona unahisi kukwazika, SASA SWALI NI KWAMBA, JE? walipaswa kuwa sawa kama ulivyotaka au walipaswa kufuata matamanio yao binafsi, Ukiepusha ushauri wa mtu kuwa mfuasi wa Iman, au Deen, basi mengine yoote ambayo ni matamanio yetu binafsi hayapaswi kurithiwa na watu wengine, haijalishi ni ndugu, rafiki au hata mtoto wako.  WANASEMA, SIKU HIZI mtoto huyu anafuata mambo yake tu, au Rafiki yangu simuelewi kwani siku hizi hafanani na mimi. WAPO WENGI WANATAMANI KUWAFANYA WENGINE KUFANANA NAO, nafikiri ni kosa la kimkakati linalotokea tangu wazazi wetu wanapotuzaa,kututunza, na kutuongoza sisi ambao ni watoto wao. Iwe kheri kwenu nyote, kwamba, Hakuna Tabia(ndoto) iliyo ya lazima kurithi.  Unaweza kufaulu kumfanya mtu kuwa kama wewe kwa kiasi fulani, lakini kukutana changamoto kama zako akanasa n

MAMBO 4 YA KUACHA SASA ILI UWE MSHINDI.

 Na, Brightermango. MAMBO 4 YA KUACHA SASA ILI UWE MSHINDI.  1. ACHA KUANDAMANA NA WATU WASIO SAHIHI. Maisha haya ni mafupi kiasi kuwa kama tutaruhusu namna yoyote kuwa na watu ambao muda mwingi wanakurudisha nyuma haiwezi kamwe kuwa sawa au na usaidizi badala yake tutaambulia hasara kubwa. Ishara ya wazi  ya watu hao, mara zote wana kuwa na wewe kwenye muda wako wa juu wa mafanikio lakini ukianza kushuka hutomuona yeyote kati yao.   Anza kuandamana na watu sahihi: hawa ni wale tu ambao wanatambua mchango wako na kuelewa zaidi hata kama hujawaeleza kukuhusu. photo: Employment page. 2. ACHA KUKWEPA AU KUKIMBIA MATATIZO YAKO. Saa chache unapokutana na tatizo huwa unapatwa na hofu... lakini kumbuka kadiri unavyojiimarisha zaidi katika kutatua changamoto ndivyo unavyokomaa kukabili nafasi za juu na kubwa hapo mbeleni aidha kwenye ajira au binafsi. ...Jaribu sasa kupambana nayo; Ukweli ni kwamba hata kama ungepaa juu zaidi na kuishi huko ulikokwenda huwezi kukwepa matatizo yanayokuhusu wewe

SIRI|| KUFANIKIWA NI KUSUBIRI.

 Na brightermango. VIPI UMEJARIBU KILA KITU LAKINI  BADO TU UNAKWAMA? Hapana, hujajaribu kila kitu, JE? umejaribu kuendelea kusubiri zaidi. Kuna wakati tunatamani mambo yaliyo juu ya upeo wetu, na tukishauriwa mara nyingi tunagundua hatukupaswa kuyatamani na badala yake kutafuta uwezo kwanza wa kuwa pale kama wahusika, yaani ninachokisema ni kwamba; "TUNAPOTAMANI KUWA KWENYE SHEREHE YA KUHITIMU ELIMU YA CHUO, BASI TULIPASWA KUWA WANACHUO AU WAHUSIKA KWA NAMNA FULANI" au "HUWEZI TUNUKIWA MEDANI KAMA HUKUSHIRIKI MASHINDANO HUSIKA" Basi ndivyo ilivyo kwenye maisha, Yaani ukiyahitaji mambo fulani hapa duniani, jitahidi ujue vigezo vyake ili na wewe uweze kuwa kama vigezo vinavyokutaka. Sasa kwenye hili letu la kujaribu kila kitu lakini bado husogei, Je? Ndio haiwezekani tena wewe kuinuka juu na kufanya mambo yako kwa mafakio? Nifuate kuna kitu leo nitakufunza,... NGOJA TUCHIMBE BUSARA ZA MABABU. Kutoka kwenye kitabu cha THE LIFE, Kinachohusika na uandishi wa