Skip to main content

MAMBO 4 YA KUACHA SASA ILI UWE MSHINDI.

 Na,

Brightermango.


MAMBO 4 YA KUACHA SASA ILI UWE MSHINDI. 

1. ACHA KUANDAMANA NA WATU WASIO SAHIHI.

Maisha haya ni mafupi kiasi kuwa kama tutaruhusu namna yoyote kuwa na watu ambao muda mwingi wanakurudisha nyuma haiwezi kamwe kuwa sawa au na usaidizi badala yake tutaambulia hasara kubwa. Ishara ya wazi  ya watu hao, mara zote wana kuwa na wewe kwenye muda wako wa juu wa mafanikio lakini ukianza kushuka hutomuona yeyote kati yao.

  Anza kuandamana na watu sahihi: hawa ni wale tu ambao wanatambua mchango wako na kuelewa zaidi hata kama hujawaeleza kukuhusu.


photo: Employment page.


2. ACHA KUKWEPA AU KUKIMBIA MATATIZO YAKO.

Saa chache unapokutana na tatizo huwa unapatwa na hofu... lakini kumbuka kadiri unavyojiimarisha zaidi katika kutatua changamoto ndivyo unavyokomaa kukabili nafasi za juu na kubwa hapo mbeleni aidha kwenye ajira au binafsi.

...Jaribu sasa kupambana nayo; Ukweli ni kwamba hata kama ungepaa juu zaidi na kuishi huko ulikokwenda huwezi kukwepa matatizo yanayokuhusu wewe pekee.

kuyatatua matatizo yako kuna andaa namna mpya yako na ziaidi kama utazitatua sawasawa basi utafikia hatua ya kuwa wewe ni bora sana.

Kuna watu wanasema " Heri nusu shari kuliko shari kamili" lakini hapa ili ubaki mshindi usikwepe matatizo yako zaidi wewe pambania kwenda mbele.

Hakikisha unatatua matatizo yako ili uwe imara zaidi kuelekea hatua ngumu zaidi.


3. ACHA KUJIDANGANYA.

Kuwa mkweli na muwazi ni kazi ngumu sana kwa mwanadamu ambaye kila wakati anatamani kuwa na thamani hapa duniani kitu ambacho kinafisha utu ule wa ndani tulio nao kiasili na hivyo kupelekea mambo mengi tuzidi au tuendelee kujidanganya.

Uongo mwingi upo hapa.. kwenye hali ya kimaisha, ukwasi na pia imani.

Maswali muhimu unayopaswa kuyakumbuka ni

 1. Je? niliyoyasema leo ni kweli.

 2.Ni kweli kwamba niko sawa kwa hili ninalolifanya.?

 3 . Hivi ninavyoonekana hapa hadharani ndivyo ninavyojiona nikiwa peke yangu?

4. Mara ngapi nimetengeneza furaha au chuki kwa watu wanaonizunguka?

...Anza Kuwa muwazi na mkweli kwako, jiambie nini kiko sawa kwako na nini hakiko sawa kwako.. watu wanapoamua kuruhusu fikra chanya basi ndipo wanapokuwa washindi.

photo from: pinterest.

4. ACHA KUYAWEKA MAHITAJI YAKO NYUMA.

Kama hujui kitu kinachouma sana ni vile unavyopotea wewe kipindi unataka kumfurahisha mwingine. ukiweka mbele maisha yako haina maana wewe ni mbinafsi.. Ebu fikiri hili... kama ukiweka nafasi ya mbele mafanikio ya rafiki zako, ni lini utafanya au hata kufikiri kuhusiana na vitu vinavyoweza kukufanikisha. Yapo ambayo labda huyajui.. kwa kawaida watu huyahesabu mafanikio katika kona zao binafsi... wapo wanaamini ni kutembea dunia nzima, wengine kuwa ni kuoa mwanamke mrembo zaidi, wengine wanaamini ni kuwajengea msingi mwema watoto au wazazi wao wa kimaisha na lakini zaidi wengine mafanikio yao wengine ni kuwa na ukwasi au fedha nyingi.


      photo credit: enchantingminds

Comments

Post a Comment

Popular posts from this blog

UMUHIMU WA NDOTO.

 Brightermango. KILA MTU ATIMIZE NDOTO ZAKE, SIO LAZIMA WOTE WAWE KAMA WEWE.  Inauma  sana pale unapoona mtu au kundi la watu, wanapoenda kinyume na vile ulivyotamani kuwaona. Kila wakati yamkini ukiwaona unahisi kukwazika, SASA SWALI NI KWAMBA, JE? walipaswa kuwa sawa kama ulivyotaka au walipaswa kufuata matamanio yao binafsi, Ukiepusha ushauri wa mtu kuwa mfuasi wa Iman, au Deen, basi mengine yoote ambayo ni matamanio yetu binafsi hayapaswi kurithiwa na watu wengine, haijalishi ni ndugu, rafiki au hata mtoto wako.  WANASEMA, SIKU HIZI mtoto huyu anafuata mambo yake tu, au Rafiki yangu simuelewi kwani siku hizi hafanani na mimi. WAPO WENGI WANATAMANI KUWAFANYA WENGINE KUFANANA NAO, nafikiri ni kosa la kimkakati linalotokea tangu wazazi wetu wanapotuzaa,kututunza, na kutuongoza sisi ambao ni watoto wao. Iwe kheri kwenu nyote, kwamba, Hakuna Tabia(ndoto) iliyo ya lazima kurithi.  Unaweza kufaulu kumfanya mtu kuwa kama wewe kwa kiasi fulani, lakini kukutana changamoto kama zako akanasa n

SIRI|| KUFANIKIWA NI KUSUBIRI.

 Na brightermango. VIPI UMEJARIBU KILA KITU LAKINI  BADO TU UNAKWAMA? Hapana, hujajaribu kila kitu, JE? umejaribu kuendelea kusubiri zaidi. Kuna wakati tunatamani mambo yaliyo juu ya upeo wetu, na tukishauriwa mara nyingi tunagundua hatukupaswa kuyatamani na badala yake kutafuta uwezo kwanza wa kuwa pale kama wahusika, yaani ninachokisema ni kwamba; "TUNAPOTAMANI KUWA KWENYE SHEREHE YA KUHITIMU ELIMU YA CHUO, BASI TULIPASWA KUWA WANACHUO AU WAHUSIKA KWA NAMNA FULANI" au "HUWEZI TUNUKIWA MEDANI KAMA HUKUSHIRIKI MASHINDANO HUSIKA" Basi ndivyo ilivyo kwenye maisha, Yaani ukiyahitaji mambo fulani hapa duniani, jitahidi ujue vigezo vyake ili na wewe uweze kuwa kama vigezo vinavyokutaka. Sasa kwenye hili letu la kujaribu kila kitu lakini bado husogei, Je? Ndio haiwezekani tena wewe kuinuka juu na kufanya mambo yako kwa mafakio? Nifuate kuna kitu leo nitakufunza,... NGOJA TUCHIMBE BUSARA ZA MABABU. Kutoka kwenye kitabu cha THE LIFE, Kinachohusika na uandishi wa