Skip to main content

MAISHA NI SAFARI NA HAKIKA NAULI HULIPWA MWISHO.

 Brightermango.

LAU KAMA TUNGEJUA MAISHA NI SAFARI NA NAULI TUNALIPA MWISHO..
Basi tusingechukiana pasipo sababu, wala kusemana (backbitting) hata kama sababu zingekuwepo basi kwa upendo tungeelezana na pasipo chuki tungerekebishana.
IBADA tungefanya kwa uaminifu mkubwa, walio Wakristo, Misingi ya Imani tungeifuata na kukumbushana huku tukiusiana juu ya siku ile ya Mwisho ya Kiama.

KWA MUSLIMS pia tusingekubali kufanya Ibada peke yetu na tungejifunza dini sana ili kwa nafasi zetu tukusanye nauli za kutosha, Maana ni adhabu kubwa kiasi gani kwa anayeitaliki swala,  Heri mtu yule aionaye njia ya ibada na kuiendea kuliko yule anayejawa na kibri na ukaidi.


MSAADA; siku zote tungekuwa wa kwanza kuwasaidia wanaotuzunguka kwani tungejua ya kuwa vyoote na yote tulinayo hayatoshi Kulipia SAFARI YETU na hivyo tungetaka nyongeza kwenye mali na kila kitu chetu.

WATOTO YATIMA,Kamwe tusingefurahi kuwepo maneno kama "Watoto wa Mitaani" Ilhari tuko na nafasi na uwezo wa kuwatunza, na zaidi tungeondoa kabisa maeneo ya wao kutunzwa na kuishi nao kwenye majumba yetu.
  SAFARI NI SAFARI, Kwa hiyo tusingekubali kubaki nyuma wakati wa kuondoka, na tusingeondoka kama tunahama hivi, bali tungekuwa na wasaa wa kuwapa nafasi zetu wengine waliobaki kwa kuwaelekeza tulivyofanya.
TUSINGE DHULUMU, kama tulivyo waliowengi, huwa tuko bize kuomba punguzo la nauli, kama tungegundua tu kuwa maisha haya ni safari basi tusingeomba punguzo na badala yake tungehitaji zaidi maandalizi ya pesa za kutosha ili tufike salama salimini tukiwa tume keti na tuko tayari.
  KUFA, kusingekuwa kitisho chochote kwani tungetambua ya kuwa huo ndio wakati sahihi wa kuondoka ndani ya lile Gari la safari.
JITAFAKARI, BAADA YA KUFIKA HUKO MWISHO, NAULI UNGEKUWA NAYO YA KULIPIA WALAU KWA KIWANGO CHA KAWAIDA NA SIO KILE CHA LUXURY.

Sidhani kama wote tuko tayari kwa Nauli,, ila cha muhimu Turudi nyuma na kujipanga kwa kurekebisha pale tunapohisi tumekwama na hatimae tuvuke au tusafiri kwa amani tukiwa na NAULI ya safari hii ndefu ya hapa Duniani.
Basi tuwausie na wengine kwa kushirikisha andiko hili.

Kwa Tafakuri kama hizi, nifuate/Nifollow.
Mimi
Brighter Mango

Page yangu
Brightermango purpose
GROUP NI
↪BRIGHTERMANGO
contact +255747270003.

#SHARE

Comments

Popular posts from this blog

UMUHIMU WA NDOTO.

 Brightermango. KILA MTU ATIMIZE NDOTO ZAKE, SIO LAZIMA WOTE WAWE KAMA WEWE.  Inauma  sana pale unapoona mtu au kundi la watu, wanapoenda kinyume na vile ulivyotamani kuwaona. Kila wakati yamkini ukiwaona unahisi kukwazika, SASA SWALI NI KWAMBA, JE? walipaswa kuwa sawa kama ulivyotaka au walipaswa kufuata matamanio yao binafsi, Ukiepusha ushauri wa mtu kuwa mfuasi wa Iman, au Deen, basi mengine yoote ambayo ni matamanio yetu binafsi hayapaswi kurithiwa na watu wengine, haijalishi ni ndugu, rafiki au hata mtoto wako.  WANASEMA, SIKU HIZI mtoto huyu anafuata mambo yake tu, au Rafiki yangu simuelewi kwani siku hizi hafanani na mimi. WAPO WENGI WANATAMANI KUWAFANYA WENGINE KUFANANA NAO, nafikiri ni kosa la kimkakati linalotokea tangu wazazi wetu wanapotuzaa,kututunza, na kutuongoza sisi ambao ni watoto wao. Iwe kheri kwenu nyote, kwamba, Hakuna Tabia(ndoto) iliyo ya lazima kurithi.  Unaweza kufaulu kumfanya mtu kuwa kama wewe kwa kiasi fulani, lakini kukutana changamoto kama zako akanasa n

MAMBO 4 YA KUACHA SASA ILI UWE MSHINDI.

 Na, Brightermango. MAMBO 4 YA KUACHA SASA ILI UWE MSHINDI.  1. ACHA KUANDAMANA NA WATU WASIO SAHIHI. Maisha haya ni mafupi kiasi kuwa kama tutaruhusu namna yoyote kuwa na watu ambao muda mwingi wanakurudisha nyuma haiwezi kamwe kuwa sawa au na usaidizi badala yake tutaambulia hasara kubwa. Ishara ya wazi  ya watu hao, mara zote wana kuwa na wewe kwenye muda wako wa juu wa mafanikio lakini ukianza kushuka hutomuona yeyote kati yao.   Anza kuandamana na watu sahihi: hawa ni wale tu ambao wanatambua mchango wako na kuelewa zaidi hata kama hujawaeleza kukuhusu. photo: Employment page. 2. ACHA KUKWEPA AU KUKIMBIA MATATIZO YAKO. Saa chache unapokutana na tatizo huwa unapatwa na hofu... lakini kumbuka kadiri unavyojiimarisha zaidi katika kutatua changamoto ndivyo unavyokomaa kukabili nafasi za juu na kubwa hapo mbeleni aidha kwenye ajira au binafsi. ...Jaribu sasa kupambana nayo; Ukweli ni kwamba hata kama ungepaa juu zaidi na kuishi huko ulikokwenda huwezi kukwepa matatizo yanayokuhusu wewe

SIRI|| KUFANIKIWA NI KUSUBIRI.

 Na brightermango. VIPI UMEJARIBU KILA KITU LAKINI  BADO TU UNAKWAMA? Hapana, hujajaribu kila kitu, JE? umejaribu kuendelea kusubiri zaidi. Kuna wakati tunatamani mambo yaliyo juu ya upeo wetu, na tukishauriwa mara nyingi tunagundua hatukupaswa kuyatamani na badala yake kutafuta uwezo kwanza wa kuwa pale kama wahusika, yaani ninachokisema ni kwamba; "TUNAPOTAMANI KUWA KWENYE SHEREHE YA KUHITIMU ELIMU YA CHUO, BASI TULIPASWA KUWA WANACHUO AU WAHUSIKA KWA NAMNA FULANI" au "HUWEZI TUNUKIWA MEDANI KAMA HUKUSHIRIKI MASHINDANO HUSIKA" Basi ndivyo ilivyo kwenye maisha, Yaani ukiyahitaji mambo fulani hapa duniani, jitahidi ujue vigezo vyake ili na wewe uweze kuwa kama vigezo vinavyokutaka. Sasa kwenye hili letu la kujaribu kila kitu lakini bado husogei, Je? Ndio haiwezekani tena wewe kuinuka juu na kufanya mambo yako kwa mafakio? Nifuate kuna kitu leo nitakufunza,... NGOJA TUCHIMBE BUSARA ZA MABABU. Kutoka kwenye kitabu cha THE LIFE, Kinachohusika na uandishi wa