Na brightermango.
VIPI UMEJARIBU KILA KITU LAKINI BADO TU UNAKWAMA?
Hapana, hujajaribu kila kitu, JE? umejaribu kuendelea kusubiri zaidi.
Kuna wakati tunatamani mambo yaliyo juu ya upeo wetu, na tukishauriwa mara nyingi tunagundua hatukupaswa kuyatamani na badala yake kutafuta uwezo kwanza wa kuwa pale kama wahusika, yaani ninachokisema ni kwamba; "TUNAPOTAMANI KUWA KWENYE SHEREHE YA KUHITIMU ELIMU YA CHUO, BASI TULIPASWA KUWA WANACHUO AU WAHUSIKA KWA NAMNA FULANI" au "HUWEZI TUNUKIWA MEDANI KAMA HUKUSHIRIKI MASHINDANO HUSIKA"
Basi ndivyo ilivyo kwenye maisha, Yaani ukiyahitaji mambo fulani hapa duniani, jitahidi ujue vigezo vyake ili na wewe uweze kuwa kama vigezo vinavyokutaka.
Sasa kwenye hili letu la kujaribu kila kitu lakini bado husogei, Je? Ndio haiwezekani tena wewe kuinuka juu na kufanya mambo yako kwa mafakio?
Nifuate kuna kitu leo nitakufunza,...
NGOJA TUCHIMBE BUSARA ZA MABABU.
Kutoka kwenye kitabu cha THE LIFE, Kinachohusika na uandishi wa vitabu vinavyoonyesha maisha ya wazi waliowahi kuishi watu mashuhuri, KILINUKUU KAULI YA Bruce Lee
"HAKUNA SIRAHA YENYE NGUVU ZAIDI YA NIA",
Akimaanisha #NIA ndio siraha imara kwa ajili ya kila vita kwenye haya, maisha kwa wasiomjua huyu alikuwa ni mwalimu wa ngumi aina ya #Wingchun na baadae aliboresha staili ile na kugundua staili yake ya ngumi mpya aliyoiita #jeetkundo huku akifanya
Midaharo iliyoruhusu mapambano ya ngumi dhidi ya wale waliobeza elimu yake ya ngumi, pia anakumbukwa kuwa mwanafalsa mwenye upeo mkubwa wa kufanya maamuzi, zaidi ya yote alikuwa muigizaji wa picha za Ngumi, kwa reference nimekuwekea picha hapo chini.
BAADA YA MUNGU SASA LINALOFUATIA NI HILI LA KUTIA #NIA.
#NIA ilimfanya Sr Ramanujan kusafiri kutoka INDIA ya kusini hadi Uingereza akisaidiwa na Mr littlewood ili tu achapishe Andiko lake la hisabati la "Infinte series".
#NIA ilimfanya Adolf hitler akwee mpaka juu na kufanya aliyoyafanya.
#NIA Ndio ilitufungulia dunia ya wireless, kutoka kwa MSERBIA NIKOLA TESLA, ambae baadae sana alihamia marekani na zaidi kugundua Ac motor, na kurahisisha usafirishaji wa umeme kwa haraka zaidi ya ile aliyokuwa anatumia Sir Thomas Edison Alva, pia huyu kaboresha sekta ya ulinzi kwa kugundua nyambizi( torpedo ), Remote controller... pia ndiye aliyeboresha radio wave transmission na mengine mengi.
#NIA Ilimfanya Mahatma kutokuwa na amani mpaka alipowakomboa Wahindi.
#NIA ilimpeleka ikulu Nelson Mandela baada ya zaidi ya miongo kadhaa kwenye mapambano.
CONT.. 0747270003
UNAHITAJI #NIA ILI UFANIKIWE.
Comments
Post a Comment