Skip to main content

UMUHIMU WA NDOTO.

 Brightermango.

KILA MTU ATIMIZE NDOTO ZAKE, SIO LAZIMA WOTE WAWE KAMA WEWE.

 Inauma  sana pale unapoona mtu au kundi la watu, wanapoenda kinyume na vile ulivyotamani kuwaona. Kila wakati yamkini ukiwaona unahisi kukwazika, SASA SWALI NI KWAMBA, JE? walipaswa kuwa sawa kama ulivyotaka au walipaswa kufuata matamanio yao binafsi, Ukiepusha ushauri wa mtu kuwa mfuasi wa Iman, au Deen, basi mengine yoote ambayo ni matamanio yetu binafsi hayapaswi kurithiwa na watu wengine, haijalishi ni ndugu, rafiki au hata mtoto wako.


 WANASEMA, SIKU HIZI mtoto huyu anafuata mambo yake tu, au Rafiki yangu simuelewi kwani siku hizi hafanani na mimi. WAPO WENGI WANATAMANI KUWAFANYA WENGINE KUFANANA NAO, nafikiri ni kosa la kimkakati linalotokea tangu wazazi wetu wanapotuzaa,kututunza, na kutuongoza sisi ambao ni watoto wao.


Iwe kheri kwenu nyote, kwamba, Hakuna Tabia(ndoto) iliyo ya lazima kurithi. 

Unaweza kufaulu kumfanya mtu kuwa kama wewe kwa kiasi fulani, lakini kukutana changamoto kama zako akanasa na kushindwa kufanikiwa kuikwepa changamoto hiyo.

NA HII NDIO SABABU KWENYE FAMILIA KUNA MMOJA ANA JIHESHIMU NA MWINGINE HAJIHESHIMU.

YUPO yule ana MITUSI MINGI MDOMONI, japo kwao hawatukani na wamejaribu kumnyoosha imeshindikana.


HII ndio sababu ambayo wengi tunatamani kuwabadilisha ndugu zetu, kwa kipindi cha udogo wao wanatutii lakini wakiwa wakubwa wanachukua njia nyingine.

JAPO SIO KOSA, SISEMI KUWA SIO HALALI KUWABADILISHA AU KUWARITHISHA TABIA NJEMA.

ILA UKIONA KAIACHA NJIA, MUACHE AWE NA IKITOKEA KAENDELEA KUFANYA YAKE KWA MAFANIKIO BASI MPONGEZE, ILA KAMA ALIKOSEA NA KURUDI KUJIFUNZA BASI ACHA MLANGO WA MAZUNGUMZO WAZI.

Maana bin adamu Tumeumbwa kujikubali zaidi, Hivyo kuna wakati tunakosea kuyaona mambo mazuri kutoka kwa wale wanaotuzunguka kwa kutaka wao tu wafuate yale tunayotaka peke yetu.

 

USIJEJICHUKIA KWA KUMFANYA AWE VILE ULIVYOTAKA... KUNA WATU WAO NI MIFANO DHAHIRI KUFUATA.Lakini sio kila mtu ni mfano dhahiri wa kufuatwa.


LENGO: MALEZI YAKO YASIZUIE NDOTO ZA WANAOKUZUNGUKA.... Haijalishi kiasi gani unawapenda wanaokuzunguka, changamoto ya kuwafanya wafanye tu mambo unayoyapenda wewe peke yako inawanyima nafasi ya kuwa Huru kifikra.

MFANO: Gaidi huwa anafikiri yuko sahihi kukirithisha kizazi chake ndoto zake na kuwaanda watoto wake wawe kama yeye.

Bila kujali nini watoto wanahitaji, atawafundisha kwa lazima mbinu zake na ikibidi anaweza wauwa wakeze tu kutimiza adhma yake.

"Ila hii iko tofauti tu kwa gaidi mmoja mkolombia aliyeitwa Pablo Escobar."


PHOTO:  URIA PETER.


Comments

Popular posts from this blog

MAMBO 4 YA KUACHA SASA ILI UWE MSHINDI.

 Na, Brightermango. MAMBO 4 YA KUACHA SASA ILI UWE MSHINDI.  1. ACHA KUANDAMANA NA WATU WASIO SAHIHI. Maisha haya ni mafupi kiasi kuwa kama tutaruhusu namna yoyote kuwa na watu ambao muda mwingi wanakurudisha nyuma haiwezi kamwe kuwa sawa au na usaidizi badala yake tutaambulia hasara kubwa. Ishara ya wazi  ya watu hao, mara zote wana kuwa na wewe kwenye muda wako wa juu wa mafanikio lakini ukianza kushuka hutomuona yeyote kati yao.   Anza kuandamana na watu sahihi: hawa ni wale tu ambao wanatambua mchango wako na kuelewa zaidi hata kama hujawaeleza kukuhusu. photo: Employment page. 2. ACHA KUKWEPA AU KUKIMBIA MATATIZO YAKO. Saa chache unapokutana na tatizo huwa unapatwa na hofu... lakini kumbuka kadiri unavyojiimarisha zaidi katika kutatua changamoto ndivyo unavyokomaa kukabili nafasi za juu na kubwa hapo mbeleni aidha kwenye ajira au binafsi. ...Jaribu sasa kupambana nayo; Ukweli ni kwamba hata kama ungepaa juu zaidi na kuishi huko ulikokwenda huwezi kukwepa matatizo yanayokuhusu wewe

SIRI|| KUFANIKIWA NI KUSUBIRI.

 Na brightermango. VIPI UMEJARIBU KILA KITU LAKINI  BADO TU UNAKWAMA? Hapana, hujajaribu kila kitu, JE? umejaribu kuendelea kusubiri zaidi. Kuna wakati tunatamani mambo yaliyo juu ya upeo wetu, na tukishauriwa mara nyingi tunagundua hatukupaswa kuyatamani na badala yake kutafuta uwezo kwanza wa kuwa pale kama wahusika, yaani ninachokisema ni kwamba; "TUNAPOTAMANI KUWA KWENYE SHEREHE YA KUHITIMU ELIMU YA CHUO, BASI TULIPASWA KUWA WANACHUO AU WAHUSIKA KWA NAMNA FULANI" au "HUWEZI TUNUKIWA MEDANI KAMA HUKUSHIRIKI MASHINDANO HUSIKA" Basi ndivyo ilivyo kwenye maisha, Yaani ukiyahitaji mambo fulani hapa duniani, jitahidi ujue vigezo vyake ili na wewe uweze kuwa kama vigezo vinavyokutaka. Sasa kwenye hili letu la kujaribu kila kitu lakini bado husogei, Je? Ndio haiwezekani tena wewe kuinuka juu na kufanya mambo yako kwa mafakio? Nifuate kuna kitu leo nitakufunza,... NGOJA TUCHIMBE BUSARA ZA MABABU. Kutoka kwenye kitabu cha THE LIFE, Kinachohusika na uandishi wa